Home
»
» Unlabelled
» SERIKALI YATANGAZA KUZIBORESHA SHULE ZA MSINGI INAZOZIMILIKI
Serikali
inatarajia kuziboresha shule za msingi inazomiliki ili ziweze kuwa na
hadhi sawa na zile za mchepuo wa kiingereza zinazomilikiwa na watu
binafsi, hatua ambayo inalenga kufuta dhana ya shule hizo kubezwa kwa
madai ya kutokuwa na kiwango bora cha utoaji elimu ikilinganishwa na
shule hizo za binafsi.
Naibu
Waziri wa nchi Ofisi wa Makamu wa Rais Charles Kitwanga ametangaza
mpango huo wa Serikali wakati akizungumza na wazazi wanaojiandaa kuanza
safari ya kuwasomesha watoto wao kidato cha kwanza baada ya kuhitimu
elimu ya darasa la saba katika shule ya Msingi Nyamalango iliyopo kata
ya Mkolani wilayani Nyamagana mkoani Mwanza.
Amesema uboreshaji
huo utahusisha ukarabati wa majengo, ujenzi wa maktaba za kisasa pamoja
na uwekaji wa nishati ya Umeme huku akiziagiza kamati za shule
kuzingatia ulipaji wa gharama za umeme kwa wakati ili kuepuka usumbufu
wa kukatiwa nishati hiyo, lengo likiwa kuondoa matabaka yaliyoanza
kujitokeza katika mfumo wa elimu nchini.
Post a Comment