Home
»
» Unlabelled
» MBUNGE WA TEMEKE ABBAS MTEMVU AZITEMBELEA FAMILIA NNE ZILIZOATHIRIKA NA JANGA LA MOTO
Mbunge
wa Temeke Mkoani Dar es Salaam, Abbas Mtemvu amezitembelea na
kuzifariji familia nne zilizoathirika na janga la moto ulioteketeza
makazi yao mwanzoni mwa wiki eneo la Kichangani kata ya Azimio, Manispaa
ya Temeke jijini Dar es Salaam.
Akiambatana na Diwani wa Kata ya Azimio Khamis Mzuzuri pamoja na baadhi
ya viongozi wa mtaa na kata hiyo Bwana Mtemvu ameshuhudia athari ya
moto huo, ambao uliteketeza samani na vifaa vyote na hivi sasa
waathirika hao wanaishi kwa majirani.
Katika ziara hiyo fupi,
Bwana Mtemvu aliwakabidhi waathirika hao msaada wa vyakula na pesa
taslimu ili ziwasaidie katika kipindi hiki kigumu, huku akifanya
taratibu kuiomba halmashauri ya Manispaa ya Temeke kuangalia uwezekano
wa kutoa msaada zaidi utakaowawezesha kuendelea kuishi maisha ya
kawaida, tofauti na sasa ambapo wanahifadhiwa kwa majirani.
Post a Comment